Takriban Wapalestina tisa wameuawa katika operesheni kubwa iliyofanywa na wanajeshi wa Israel kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, wizara ya afya ya Palestina inasema.

Vikosi vya usalama vya Israel vilisema vimeanza "operesheni ya kukabiliana na ugaidi" huko Jenin na Tulkarm usiku kucha na kwamba hadi sasa wamewaua "magaidi watano wenye silaha kutoka angani na ardhini".

Pia ilisema wengine wanne waliuawa katika shambulizi la anga wakati wa operesheni ya wakati mmoja katika kambi ya wakimbizi ya al-Faraa karibu na Tubas.

Waandishi wa habari wa ndani walisema hawajaona chochote cha upeo na kiwango hiki katika Ukingo wa Magharibi tangu siku za intifada ya pili ya Wapalestina, au uasi, miongo miwili iliyopita.