Tunaweza kukuletea habari za hivi punde asubuhi ya leo wakati Urusi ikifanya mashambulizi makubwa ya anga dhidi ya Ukraine.

Msururu wa mashambulizi ya ndege zisizo na rubani na makombora yalianza kote nchini usiku wa Jumatatu.

Milipuko ilitanda katika miji kadhaa katika mikoa 15 kulingana na Waziri Mkuu wa Ukraine Maafisa wa mkoa wanasema takribani watu watatu wameuawa nchi nzima iko chini ya tahadhari ya uvamizi wa anga.

Tumeshuhudia kukatika kwa umeme huku mashambulizi ya Urusi yakilenga miundombinu ya nishati na maji.

Wakazi wa Kyiv wanatafuta makazi katika vituo vya treni .

Jirani wa Ukraine, Poland, anasema kuwa jeshi lake la anga limeanzishwa kwa sababu mashambulizi yamekaribia anga ya Poland.

Tunasikia kwamba Ukraine imekabiliana na mashambulizi ya ndege yake isiyo na rubani lakini kwa kiwango kidogo zaidi.