Rais wa Ukraine Volodymr Zelensky amesema hivi punde kuwa zaidi ya makombora 100 na takribani ndege 100 za mashambulizi zilirushwa na Urusi usiku kucha.

Anasema kuwa lengo kuu lilikuwa "miundombinu muhimu ya kiraia" katika mikoa mingi ya Ukraine, akitoa mfano wa mashambulizi dhidi ya Kharkiv, Kyiv, Odesa na maeneo ya magharibi.

Katika chapisho kwenye Telegram, Zelensky anaongeza kuwa kumekuwa na uharibifu mkubwa wa vifaa vya nishati, lakini anasema kazi ya ukarabati inaendelea na wafanyakazi "watafanya kazi ya ukarabati saa nzima".

Anaendelea kutoa wito kwa washirika wa Magharibi kuiruhusu Ukraine kutumia silaha za masafa marefu na kuwaruhusu kupiga maeneo nchini Urusi ambayo mashambulizi yanaanzishwa.