China na Ufilipino zimeshutumiana katika tukio la kugongana kwa meli za walinzi wa pwani katika eneo linalozozaniwa la Bahari ya China Kusini.

Ufilipino imedai meli ya China "moja kwa moja na kwa makusudi" iligonga meli yake, huku Beijing ikiishutumu Ufilipino kwa "kuigonga" kwa makusudi meli ya Uchina.

Mgongano wa Jumamosi karibu na eneo la Sabina ni wa hivi karibuni zaidi katika mzozo wa muda mrefu - na unaozidi kuongezeka - kati ya nchi hizo mbili juu ya visiwa na maeneo mbalimbali katika Bahari ya China Kusini.

Ndani ya wiki mbili zilizopita, kumekuwa na matukio mengine matatu katika eneo moja yanayohusisha meli za nchi hizo mbili.