Mtandao wa X, uliojulikana zamani kama Twitter, amepigwa marufuku nchini Brazil baada ya kushindwa kutimiza makataa yaliyowekwa na jaji wa Mahakama ya Juu.

Alexandre de Moraes aliamuru "kusitishwa mara moja na kikamilifu" kuendeshwa kwa mtandao huo wa kijamii hadi itii amri zote za mahakama na kulipa faini zilizopo.

Mzozo huo ulianza mwezi Aprili, huku jaji akiamuru kufungwa kwa akaunti nyingi za X kwa madai ya kueneza habari potofu.

Akijibu uamuzi huo, mmiliki wa X Elon Musk alisema: "Uhuru wa kujieleza ndio msingi wa demokrasia na hakimu bandia ambaye hajachaguliwa nchini Brazili anaiharibu kwa malengo ya kisiasa."

X inasemekana kutumiwa na moja ya kumi ya wakazi milioni 200 wa taifa hilo.

Kufikia Jumamosi asubuhi baadhi ya watumiaji walikuwa wameripoti kushindwa kuingia kwenye jukwaa hilo.

X ilifunga ofisi yake nchini Brazil mapema mwezi huu, ikisema mwakilishi wake alitishiwa kukamatwa ikiwa hatatii amri ilizozitaja kama "udhibiti" - na kwamba ni kinyume cha sheria chini ya sheria za Brazil.

Jaji Moraes alikuwa ameamuru kwamba akaunti za X zinazoshutumiwa kueneza habari potofu - lazima zizuiwe wakati zinaendelea kuchunguzwa.

Aliongeza kuwa wawakilishi wa kisheria wa kampuni hiyo watawajibishwa ikiwa akaunti yoyote itafunguliwa tena.

X imetishiwa kutozwa faini kwa kukataa kutii agizo hili, huku kampuni hiyo na Bw Musk wakiungana na wakosoaji nchini Brazil kumshutumu jaji huyo kuegemea mrengo