MAONESHO ya Kimataifa ya Utalii ‘Swahili Internation Tourist Export 2024’ yameanza leo Mlimani, Dar es Salaam na yanatarajiwa kutamatika Oktoba 13.

Akizungumza Mkurugenzi wa Kampuni ya Hanspaul Group, Satbir Singh Hanspaul ameishukuru serikali kwa kutoa kipaumbele kwa sekta binafsi na kusambaza magari ya utalii kwenye nchi 18 duniani

kote.“Kampuni ya Hanspaul Group imepata nafsi ya kusambaza magari kwenye nchi 19 kutokana na jitahada za serikali. Naahidi kuendelea kushirikiana na serikali na wadau mbalimbali kuongeza uchumi wa nchi kupitia biashara ya kampuni hiyo,”amesema.