Waandamanaji katika mji mkuu wa DRC Kinshasa wamechoma moto sehemu za ubalozi wa Ufaransa, huku wakiendelea kuonyesha kutoridhishwa na mashambulizi ya kundi la M23 mjini Goma.

Walivamia mitaa, kuzuia matembezi na mizunguko , na kuchoma matairi barabarani.

Moshi ulionekana ukifuka hewani wakati sehemu za ubalozi huo zilipokuwa zikiwaka moto.

Siku ya Jumatatu, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot alielezea mshikamano wa Ufaransa na DRC na uadilifu wake wa eneo "wakati Goma inajiandaa kuangukia."mikononi mwa waasi. Amewataka M23 kuacha mashambulizi yake.

Aliwataka M23 kuacha mashambulizi yake.