Mwanamke aliyebadilisha jinsia yake ambaye yuko gerezani amewasilisha kesi mahakamani akisema kwamba agizo la Rais Donald Trump lenye kueleza Serikali ya Marekani kutambua jinsia mbili tu, zisizobadilika na inayohitaji wafungwa kama yeye kuwekwa katika magereza ya wanaume inakiuka Katiba ya Marekani na sheria za nchi.
Katika kesi iliyowasilishwa Jumapili katika Mahakama ya Shirikisho la Boston, mfungwa huyo, ambaye anawakilishwa na mawakili katika vikundi vya kutetea haki za binadamu ikiwa ni pamoja na Mawakili na Watetezi wa LBTQ, alilenga agizo la Trump lililosainiwa siku yake ya kwanza kurudi ofisini Januari.
Kuhamishwa kwa mlalamikaji katika gereza la wanaume pia kutakiuka marufuku ya Marekebisho ya Nane ya Katiba ya Marekani dhidi ya adhabu ya kikatili na isiyo ya kawaida, na kumnyima mlalamishi huduma ya afya inayohitajika kitakiuka sheria ya shirikisho inayojulikana kama Rehabilitation Act of 1973, kulingana na kesi hiyo.
0 Comments