Mwanamuziki Britney Spears

Mwimbaji nyota wa muziki aina ya Pop Britney Spears ameuza haki za orodha yake yote ya muziki, BBC imebaini.

Spears, 44, inasemekana aliuza haki hizo kwa mchapishaji huru wa muziki wa Primary Wave tarehe 30 Desemba kwa karibu $200m (£146m).

Mwimbaji huyo - ambaye uhifadhi wake wa muda mrefu uliamuru maisha yake ya kibinafsi na kitaaluma - anajulikana kwa vibao ...Baby One More Time, Oops!... I Did It Again, Toxic na Gimme More.

Primary Wave haikujibu mara moja maombi ya BBC ya kutoa maoni.

Wawakilishi wa Spears walikataa kutoa maoni.

Mnamo Januari 2024, mwimbaji huyo alisema "hatarudi tena kwenye tasnia ya muziki".

Wimbo wake wa mwisho aliimba pamoja na mwanamuziki Elton John mnamo 2022.