Haki za binadamu zinakanyagwa kote ulimwenguni, mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema siku ya Jumatatu, akitaja ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa na mateso mabaya dhidi ya raia katika migogoro nchini Sudan, Gaza, na Ukraine.
"Utawala wa sheria unazidiwa nguvu na utawala wa mabavu," amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, akizungumza katika ufunguzi wa Baraza la Haki za Binadamu huko Geneva.
Guterres amesema haki za binadamu zinasukumwa nyuma kimakusudi, akizitaka nchi wanachama kutoziona haki za binadamu kama orodha ya kuchagua.
Guterres ametete mfumo wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa ambao uko katika changamoto kutokana na kupungua kwa ufadhili, mashambulizi dhidi ya baadhi ya wataalamu wake na kujiondoa kwa Marekani katika mifumo muhimu ya uwajibikaji juu ya haki za binadamu.
"Mahitaji ya kibinadamu yanaongezeka huku ufadhili ukiporomoka," amesema.
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, kama sehemu zingine za shirika hilo, inakabiliwa na mdororo wa bajeti kufuatia uamuzi wa kupunguzwa kwa ufadhili kutoka Marekani - mfadhili mkuu wa Umoja wa Mataifa - pamoja na serikali zingine.

0 Comments