Iran imeonyesha kuwa iko tayari kufanya makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia katika mazungumzo na Marekani ili kuondoa vikwazo na kutambua haki yake ya kurutubisha urani, huku ikijaribu kuzuia shambulio la Marekani.
Wachambuzi wanasema hatua hiyo inaonyesha kwamba Tehran inataka diplomasia ili kuzuia shambulio kubwa la Marekani.
Afisa huyo amesema Tehran itazingatia uwezekano wa kuondoa nusu ya urani yake iliyorutubishwa na kuipeleka nje ya nchi, kupunguza kiasi kilichobaki na kushiriki katika kuunda muungano wa kikanda kuhusu urani.
Iran itafanya hivi ikiwa Marekani itatambua haki ya Iran ya "kurutubisha urani kwa matumizi ya kiraia " chini ya makubaliano ambayo pia yatajumuisha kuondoa vikwazo vya kiuchumi, afisa huyo amesema.
Zaidi ya hayo, Iran imetoa fursa kwa makampuni ya Marekani kushiriki kama wakandarasi katika viwanda vikubwa vya mafuta na gesi vya Iran, afisa huyo amesema.
"Ndani ya makubaliano hayo Marekani pia imepewa fursa za uwekezaji mkubwa na maslahi yanayoonekana ya kiuchumi katika sekta ya mafuta ya Iran," amesema afisa huyo.
Ikulu ya White House bado haijatoa kauli kuhusu suala hilo.

0 Comments