Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov amesema Jumatano kwamba vikwazo vipya vya Marekani kuhusu jukumu la Urusi na nchi zingine katika biashara ya mafuta ya Venezuela ni ubaguzi wa wazi.

Urusi ilisema mapema Jumatano kwamba Moscow ilipanga kutafuta ufafanuzi kutoka Marekani kuhusu vikwazo hivyo vipya.

Wizara ya Fedha ya Marekani siku ya Jumanne ilitoa leseni ya jumla ili kuwezesha utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi nchini Venezuela. Leseni hiyo haikuidhinisha miamala inayohusisha raia au vyombo vya Urusi na China.

Lavrov alisema Urusi ilikuwa inawasiliana na Marekani kuhusu suala hilo na ilitaka ushirkiano unaoheshimu pande zote "bila wazo la kutawala".