Waziri wa masuala ya kigeni wa Iran, Abbas Araghchi, amesema katika mahojiano na Alaraby Aljadeed kwamba Mojtaba Khamenei yuko salama na mwenye afya njema" na "anaongoza kikamilifu."

Itakumbukwa kwamba, Mojtaba hakujitokeza hadharani tangu uteuzi wake mnamo 8 Machi.

Hotuba yake ya kwanza kwa umma ilirushwa na vyombo vya habari vya serikali mnamo 12 Machi, ikasomwa na mtangazaji.

Araghchi amesema kuwa Iran inakaribisha “mpango wowote wa kikanda ambao utaweza kuleta mwisho wa haki wa vita,” na Bahari ya Hormuz “iko wazi kwa kila mtu isipokuwa meli za Marekani na washirika wake.”

Aidha, Araghchi amesema kuwa “hakuna mpango maalum ulio mezani hadi sasa wa kumalizia vita.”