Idadi ya vifo nchini Lebanon kutokana na mapigano na Israel imeongezeka hadi watu 394, kulingana na waziri wa afya wa serikali.
Katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Jumapili, Rakan Nasserdine alisema waliofariki ni pamoja na watoto 83 na wanawake 42 tangu Lebanon ilipoanza kuhusika na vita kati ya Marekani na Israeli na Iran.
Nasserdeddine aliongeza kuwa wafanyakazi tisa wa uokoaji pia wamefariki.
Jumla ya vifo nchini Lebanon imeongezeka ikilinganishwa na Jumamosi, wakati waziri wa afya aliposema idadi hiyo ni watu 294.

0 Comments