
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika (WHO AFRO), Profesa Mohamed Janabi ambapo walijadili masuala mbalimbali ya maendeleo, hususan ushirikiano katika sekta ya afya barani Afrika.
Pia, Dkt. Mwigulu alikutana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Balozi Stephen Mbundi pamoja na Katibu Mkuu wa Jukwaa la Mabunge ya Ukanda wa Maziwa Makuu Afrika (FP-ICGLR), Balozi Dkt. Deo Mwapinga.
Mazungumzo hayo yamefanyika kando ya Mkutano wa 61 wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), unaoendelea jijini Brazzaville, Jamhuri ya Kongo leo Jumatano Mei 27, 2026.




0 Comments