
Bei ya mafuta imepanda kwa takriban dola mbili baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kuahidi kuishambulia Iran "vikali" kwa mashambulizi mapya, na kuchukua udhibiti wa masoko yake ya mafuta na gesi.
Bei ya mafuta ghafi iliongezeka hadi $94.16 kwa pipa ndani ya dakika chache alasiri ya leo, kabla ya kurudi chini kidogo.
"Hivi karibuni, tutachukua Kisiwa cha Kharg, na maeneo mengine ya miundombinu ya mafuta, na kuchukua udhibiti kamili wa Masoko yao ya Mafuta na Gesi, kama tulivyofanya Venezuela, ambayo inafanya kazi vizuri sana kwa Venezuela na Marekani," Trump aliandika kwenye mtandao wake wa Truth Social.
Mapema Alhamisi, bei ya mafuta ilikuwa imeshuka kidogo kutoka zaidi ya $95 baada ya saa 01:00 BST, hadi chini kidogo ya $92 ifikapo saa sita mchana kwa saa za Uingereza.
0 Comments