Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, amesema kuwa kufunguliwa kwa mlango bahari Hormuz ni sharti la kwanza kwa mazungumzo na Iran, lakini pekee yake haitoshi kuondolewa kwa vikwazo vya kiuchumi.
Rubio alisema kuwa moja ya masharti muhimu ya kupunguza au kuondoa vikwazo ni Iran kujitolea kushiriki mazungumzo maalumu kuhusu akiba yake ya urani iliyorutubishwa kwa kiwango cha juu.
Pia alitangaza kuwa mazungumzo kati ya Marekani na Iran yataendelea, lakini akasisitiza kuwa hakuna uhakika kwamba mazungumzo hayo yataleta amani.
Wakati huo huo, shirika la habari la Fars limeripoti kuwa kubadilishana ujumbe kati ya Iran na Marekani “kumesimama kwa angalau siku chache zijazo.”
Katika maendeleo mengine, licha ya juhudi za Donald Trump za kuingilia kati, mapigano ya kurushiana makombora na mashambulizi kati ya Israel na Hezbollah katika maeneo ya mpakani yanaendelea.
0 Comments