Maafisa wa Marekani na Iran wamewasili Uswizi kwa mazungumzo ya moja kwa moja baada ya kusaini makubaliano ya awali ya kumaliza vita wiki iliyopita.
Makubaliano hayo yanajumuisha ahadi ya kufikia makubaliano ya mwisho ndani ya siku 60, pamoja na kusitisha mapigano katika maeneo yote ya mzozo, ikiwemo Lebanon, na kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz.
Hata hivyo, mapigano yanayoendelea kati ya Israel na Hezbollah inayoungwa mkono na Iran nchini Lebanon yaliifanya Iran kutangaza Jumamosi kwamba imefunga njia hiyo muhimu ya usafirishaji wa majini, ingawa takwimu za ufuatiliaji zinaonyesha kuwa meli zimeendelea kupita katika eneo hilo.
Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, alisema kuwa Marekani ina matumaini ya kupiga hatua katika suala la nyuklia na hali ya Lebanon, huku Tehran ikisema kuwa itasisitiza upande mwingine kutekeleza ahadi zake.
Vance aliungana na wenzake nchini Uswisi Jared Kushner, mkwe wa Rais wa Marekani Donald Trump, pamoja na mjumbe maalum Steve Witkoff.
Kwa upande wa Iran, Spika wa Bunge Mohammad Bagher Ghalibaf na Waziri wa Mambo ya Nje Abbas Araghchi waliwasili nchini Uswisi Jumamosi usiku.
0 Comments