Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na waasi wa M23 wamekubaliana kuendelea na mazungumzo ya kutafuta amani, lakini bado hawajakubaliana kuhusu baadhi ya mambo muhimu.
Zimekubaliana mpango unaoonyesha hatua na muda wa kuendelea na mazungumzo yaliyokuwa yakifanyika chini ya makubaliano ya amani ya Doha, Qatar.
Pia wamekubaliana kuanza kutumia mfumo maalum wa kufuatilia kama kuna ukiukaji wa usitishaji mapigano.
Ukaguzi wa kwanza unatarajiwa kufanyika Jumatatu katika eneo la Minembwe, Kivu Kusini, ambalo limeathiriwa na mapigano.
Hata hivyo, bado hawajakubaliana kuhusu baadhi ya masuala, yakiwemo vikwazo dhidi ya M23 na kuachiwa kwa baadhi ya watu waliokamatwa.
Wakati mazungumzo yakiendelea, mapigano bado yanaendelea katika maeneo ya Kisu Kaskazini na Kivu Kusini, huku serikali na M23 zikituhumiana kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano.
Mzozo huo pia umeendelea kuongeza mvutano kati ya DRC na Rwanda. Rwanda inasema serikali ya DRC inashindwa kuliondoa kundi la FDLR, ambalo Kigali inaliona kuwa tishio kwa usalama wake.
DRC, kwa upande wake, inaituhumu Rwanda kuiunga mkono M23 kwa wanajeshi na silaha.
Rwanda inakanusha madai hayo. Mapigano hayo yamesababisha mamilioni ya watu kuondoka katika makazi yao.
0 Comments