Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ana "maswali ya kujibu" kuhusu ufisadi serikalini mwake, kulingana na kauli ya aliyekuwa Waziri wa Ulinzi, Mykhailo Fedorov, alipozungumza na BBC.

Fedorov, waziri maarufu aliyeleta mageuzi ya kisasa katika jeshi na kuanzisha matumizi ya ndege zisizo na rubani vitani, alifutwa kazi mwezi uliopita baada ya kudaiwa kutofautiana na mkuu wa jeshi la Ukraine.

Aliiambia BBC kuwa uchunguzi kuhusu utakatishaji fedha uliotangazwa wiki iliyopita umezua maswali iwapo Zelensky alikuwa na taarifa za ufisadi miongoni mwa wandani wake.

Pia Fedorov alisisitiza kuwa "demokrasia haipaswi kuwa mateka wa Putin" - lakini hakuweka wazi azma yake ya kisiasa, siku chache baada ya kuweka mtandaoni video inayotoa wito wa kutaka uchaguzi ufanywe nchini Ukraine.

Maandamano ya yalizuka nchini Ukraine kupinga kuftwa kwake lakini uungwaji mkono wake ulipungua na maandamano yalikommeshwa Jumatano, baada ya kuthibitishwa kwa nafasi ya Fedorov.

Wito wake wa uchaguzi ya wakati wa vita umepingwa kwa kiasi kikubwa.

Ukraine imekuwa chini ya sheria za kijeshi tangu uvamizi kamili wa Urusi mwaka 2022, ikimaanisha uchaguzi umesitishwa.

Fedorov ndiye mwanasiasa wa kwanza kigogo kuitisha uchaguzi mkuu ambapo kulingana na sheria za Ukraine,ni marufuku kuandaa uchaguzi wakati wa vita.