Ufaransa inajiandaa kumpokea Mrithi wa Kiti cha Ufalme na Waziri Mkuu wa Saudi Arabia, Mohammed bin Salman, kwa ziara rasmi ya siku mbili itakayoanza leo Jumapili, katika kipindi ambacho hali ya mambo katika Mashariki ya Kati ni inaendelea kuwa tete.

Kwa mujibu wa Ikulu ya Élysée, ziara hiyo inaakisi kile ilichokitaja kuwa ni "uhai wa mazungumzo" kati ya Saudi Arabia na Ufaransa, na ni fursa ya kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya nchi hizo mbili.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Mrithi wa Kiti cha Ufalme Mohammed bin Salman wanatarajiwa kufanya mkutano wa kwanza wa Baraza la Ushirikiano wa Kimkakati la Ufaransa na Saudi Arabia, ambapo watajadili masuala ya kiuchumi na kimkakati, pamoja na masuala ya kikanda.

Paris inachukulia uratibu na washirika wake wa Ghuba kuwa muhimu kwa uimarishaji wa utulivu na amani katika eneo hilo.

Macron na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia pia watashiriki katika hafla ya kufunga mashindano ya Kombe la Dunia la Michezo ya Kielektroniki (Esports World Cup), ambayo yanafanyika Paris kwa mara ya kwanza nje ya Saudi Arabia tangu mashindano hayo yalipoanzishwa.