Shirika la Nepal linalosimamia majanga limesema miili ya watu 1,287 imepatikana hadi sasa, huku ikikadiriwa kuwa watu 5,083 bado hawajulikani walipo.
Hili ni ongezeko kutoka kwa takwimu za awali zilizotolewa na polisi nchini humo, ambazo zilisema watu 1,280 walikuwa wamefariki na 4,798 walikuwa hawajulikani walipo.
Watu wawili wameokolewa wakiwa hai kutoka katika eneo lililoporomoka katika mradi wa kuzalisha umeme kwa nguvu ya maji wa Trishuli 3A nchini Nepal, siku tisa baada ya mafuriko makubwa kuikumba nchi hiyo na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 1,200.
Timu za uokoaji bado zinaendelea na juhudi za kuwaokoa watu wengine wanaodaiwa kunaswa ndani ya eneo hilo.
Suresh Raut, afisa mwandamizi wa Mamlaka ya Umeme Nepal ambaye yuko katika eneo la uokoaji, ameiambia BBC kuwa waokoaji walikuwa wakimpatia oksijeni mmoja wa watu waliookolewa, ambaye mamlaka zimemtambua kwa jina la Sanjaya Shah.
0 Comments