Waziri Mkuu nchini Israel Benjamin Netanyahu amesema siku ya Alhamisi kuwa kuuangusha utawala wa Jamhuri ya Kiislamu ni jambo "linalowezekana kufikiwa," akisisitiza kuwa utawala huo ni dhaifu kuliko wakati wowote ule na unapambana ili kusalia madarakani.
Katika hafla iliyohusisha viongozi wa kijeshi, aliongeza kuwa anaamini inawezekana "kuondoa" kabisa tishio la Iran, akilitaja hilo kuwa ndilo jukumu kuu linaloikabili Israel bado.
Netanyahu amesema kuwa hatua ya Iran kutolenga Israel katika mzunguko wa hivi karibuni wa mashambulizi haikuwa bahati mbaya, akiongeza kuwa Tehran inafahamu vyema nguvu, silaha, na azimio la Israel.
Netanyahu anajiandaa kushiriki katika uchaguzi wa bunge wenye ushindani mkali mwishoni mwa mwezi wa Oktoba.
Waziri wa Ulinzi wa Israel, Yisrael Katz, alisema nchi yake iko tayari kujibu "kwa nguvu kubwa" iwapo Iran itashambulia wakati wa sikukuu za Kiyahudi, zinazoanza katikati ya mwezi wa Septemba, akibainisha kuwa Iran ililenga maeneo mbalimbali katika eneo hilo, isipokuwa Israel, wakati wa mzozo huo wa hivi karibuni.
0 Comments