Kenya imewapa raia wa kigeni wanaoendesha biashara ndogo ndogo siku 90 za kuratibu hadhi yao ya uhamiaji, vibali vya kazi na leseni za biashara.
Katika taarifa, Msemaji wa Ikulu Hussein Mohammed alisema zoezi hilo litaratibiwa na balozi za raia walioathiriwa, na kuwapa "fursa iliyo wazi na iliyopangwa ya kuratibu" hadhi yao na shughuli za biashara.
"Katika siku 90 zijazo, Serikali itafanya zoezi la kuratibu kwa utaratibu ili kurahisisha uzingatiaji," ilisoma taarifa hiyo.
Baada ya kipindi cha siku 90, mahitaji ya uhamiaji, kibali cha kazi, usajili na leseni "yatatekelezwa kwa uthabiti na kwa ukali kulingana na sheria na mchakato unaostahili".
Tangazo hilo linafuatia agizo la awali la Rais William Ruto kwamba biashara ndogo ndogo kama vile uuzaji wa bidhaa nje na rejareja zinapaswa kutengwa kwa ajili ya Wakenya, na kusababisha wasiwasi miongoni mwa wafanyabiashara wa kigeni, haswa Warundi.
Serikali pia inatafuta kupanua Muswada wa Maudhui ya Ndani, ambao kwa sasa uko Bungeni, ili kuunda kile inachokiita "mfumo ulio wazi, wa haki na unaotabirika" wa kushiriki katika biashara ndogo ndogo.
Mabadiliko yaliyopendekezwa yatatambua shughuli za kiuchumi ambazo zinaweza kutengwa kwa ajili ya raia wa Kenya, huku yakiwalinda raia wa kigeni walio na haki halali ya kufanya kazi, kuwekeza au kufanya biashara nchini Kenya.
Serikali pia imeonya dhidi ya unyanyasaji au vitisho dhidi ya raia wa kigeni.
"Wasiwasi kuhusu fursa za kiuchumi hauwezi kamwe kuhalalisha ubaguzi, kuhalalisha uvunjaji wa sheria au kuidhinisha vurugu."
Inafuatia siku ya iliyojaa sintofahamu jijini Nairobi, ambapo mamia ya Warundi walikusanyika katika ubalozi wao huku kukiwa na hofu kuhusu agizo hilo.
Serikali ya Burundi pia iliibua wasiwasi kuhusu jinsi raia wake wanavyotendewa.
0 Comments