Masaa kadhaa baada ya meli tatu za mafuta za Iran kushambuliwa, Jeshi la Wanamaji la IRGC lilithibitisha kuwa lilifyatua makombora matatu kutoka Sirik kuelekea mlango Bahari wa Hormuz yakilenga meli kubwa ya kubeba ndege na meli ya kivita ya Marekani.
IRGC pia ilisema kuwa, ikiwa ni jibu kwa shambulio la Marekani dhidi ya meli za mafuta za Iran, ililenga meli tatu za mafuta zilizokuwa zikipita katika "njia zisizoruhusiwa kupitia mlango Bahari wa Hormuz" na pia ilishambulia meli ya kivita ya Marekani iliyokuwa ikijaribu kuingia katika mlango huo.
Marekani bado haijatoa tamko lolote kuhusu mashambulio hayo.
Mapema Jumamosi, CENTCOM ilitangaza kuwa vikosi vya Marekani vilishambulia meli tatu za mafuta za Iran.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ililaani mashambulio hayo na kusema kuwa Marekani ndiyo inayowajibika kwa matokeo ya vitendo hivyo. CENTCOM ilisema kuwa shambulio hilo lilifanyika baada ya IRGC kufyatua makombora ya balistiki dhidi ya meli mbili za kivita za Marekani.
0 Comments