Rais Jakaya Mrisho Kikwete jana amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Mabalozi wa Sweden na Norway katika hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam. Waliowasilisha hati zao ni Balozi Lennarth Hjelmaker wa Sweden na Balozi Bi.Ingunn Klepsvik wa Norway. Pichani Balozi Ingunn Klepsvik wa Norway akiwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete.