Timu ya Taifa ya Belgium (Red Devils imeshinda mechi muhimu dhidi ya timu ya Taifa ya Austria kwa goli 2 - 0 siku ya Ijumaa.Ikijiweka katika nafasi nzuri ili kusonga mbele  kwenye mashindano ya ubingwa wa Ulaya unaotarajiwa kuanzia mwakani 2012.Kocha wa timu ya Taifa ya Belgium Geogers Leekens amewaambia waandishi wa habari baada ya mechi kuisha kwamba "Hatujawaangusha ni haki yetu kushinda".