Utaratibu mzuri ambao watoto wanaelekezwa tokea wakiwa na umri mdogo.hapo unaweza kuona jinsi gani watoto wanaelekezwa jinsi ya kuweka nguo zao vizuri.
Walimu waliobobea katika malezi bora ya watoto,wakiwafunza namna ya kupanga vitu watoto shuleni,hii inampa ufahamu wa haraka mtoto jinsi ya kuweka akili yake sawa.
Ukiangalia vyema utaona facilities za watoto  ni za kutosha kabisa shuleni hapo,na hii humfanya mtoto kupenda kwenda shule bila kuhisi uvivu.mara nyingi shule zetu za watoto nyumbani Afrika hukosa mvuto wa mazingira na hivyo kumfanya mtoto kutopenda kwenda shuleni.
Nilipokuwa nchini Holland nilibahatika kutembelea shule moja ndogo ya watoto wa chekechea,pichani ni bidada Leyla Hija akiwa na sura ya furaha pindi alipoingia shuleni hapo.