Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema amesaidia kumaliza mvutano kati ya viongozi mahasimu wa Zimbabwe, baada ya kufanya ziara mjini Harare siku ya Ijumaa.
Bw Zuma amesema mzozo kati ya Rais Robert Mugabe na Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai umemalizika, baada ya saa nne za majadiliano.
Lakini wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaonya kuwa mazungumzo haya huenda yasilete matokeo ya mara moja.
Mzozo kati ya viongozi hao ni dalili ya kudorora zaidi kwa uhusiano kati ya mahasimu hao wa muda mrefu.