Kundi la wanaharakati wa kisiasa nchini Uganda maarufu kama "Activists for Change" wanatarajiwa kurejelea tena maandamano ya kutembea hadi kazini kupinga kupanda kwa bei ya mafuta na chakula.
Naye Kiongozi wa upinzani Kizza Besigye ambaye aliachiwa huru jana baada ya wiki moja rumande ameapa kuunga mkono juhudi za kundi hilo.
Ikiwa hatashiriki, hii itakuwa mara ya kwanza yanafanyika bila viongozi wa ngazi ya juu kutoka upinzani ikizingatiwa pia kuwa mwenzake, Norbert Mao wa chama cha DP yupo chini ya ulinzi.