Nchini Kenya, Waziri mkuu Raila Odinga, leo anatarajiwa kufafanua bungeni hatua serikali inachukua kudhibiti hali.
Wiki iliopita shirika linalotetea haki za wanunuzi liliandaa maandamano katika sehemu kadhaa nchini, kulaani ongezeko hilo.

Chama cha wafanyikazi kimetisha kuongoza mgomo tarehe mosi mwezi Mei mwaka huu, ikiwa mishahara ya wafanyikazi haitaongezwa, suala linalozua wasi wasi serikalini na miongoni mwa wawekezaji.