Balozi wa Korea Kusini nchini, Kim Young-Boon (wa nne kulia) akipura mpunga kwa kutumia mashine isiyotumia nishati inayojulikana kwa jina la kitaalamu ‘Thresher pedal’ baada ya ufunguzi wa banda la KOICA, kwenye Maonesho ya Nanenane yaliyoanza mjini Morogoro Agosti Mosi. Mashine hiyo hutumiwa na wakulima wa zao la mpunga vijijini nchini Korea Kusini. Wa tatu kulia ni Mkuu wa Mkoa huo, Issa Machibya. (Picha na John Nditi).