Gladness Mallya na Imelda Mtema
NYOTA wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson, anadaiwa kutumbukia kwenye vitendo vya kishirikina, Amani limenyetishiwa.
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa Aunt, mwigizaji huyo huwa ana mganga wake anayemwekea mambo sawa yanapoyumba.
“Najua mkimuuliza atabisha, lakini kwa taarifa yenu Aunt Ezekiel ni mshirikina, ana sangoma wake maalumu ambaye ni kibogoyo, anaishi Mkata mkoani Pwani.
“Huyo ndiye anayemsafishia nyota ili ang’ae kila wakati,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Kwanza Aunt akichacha huwezi kumuona mjini, huwa yuko Mkata kwa ‘babu’ kufanyiwa ‘mavituz’ na akirudi mambo yake huwa ni ng’aring’ari kwani madili yanakuwa ya kumwaga.
“Kama akibisha, muulizeni huwa anakwenda kufanya nini Mkata kwani alishanaswa mara kibao akiingia na kutoka kwa mganga wake huyo.”
Baada ya kudakishwa ‘infomesheni’ hizo, gazeti hili lilimweka ‘mtukati’ Aunt na kumwagia ‘upupu’ wote ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Kila mtu ana maisha yake hapa duniani ya namna ya kufanikiwa ambayo hayaingiliani na mwezake, yaani kwa mganga waende wao tu, tukienda sisi kwa sababu ni wasanii, basi inakuwa ni ishu?”
Hata hivyo, majibu hayo ya Aunt ndiyo yaliyozua maswali zaidi kwani hayakuweka bayana kama kilichosema ni cha kweli au la.
Skendo ya Aunt kuhusishwa na ushirikina imekuja katika kipindi ambacho kuna madai mazito kuwa tasnia ya filamu Bongo imeshikiliwa na baadhi ya mastaa wanaokesha kwa sangoma ili kukubalika na kukimbiza kwenye soko la muvi.
 

Aunt Ezekiel akiwa katika pozi.