Stori: Imelda Mtema
MKALI anayesumbua na songi la Tupogo, Omar Nyambo ‘Ommy Dimpoz’ amevuta mkoko mpya aina ya Toyota Mark-X wenye thamani ya Sh Mil 30.
Akizungumza na paparazi wetu, Ommy alisema kuwa kununua gari kwake ni moja ya matunda mazuri ya kazi yake kwa kuwa amejituma kwa muda mrefu na  kwa nguvu zote.
“Haya ni matunda ya kazi yangu nimefanya kazi na faida yake nimeiona kabisa kwa sasa hiyo ni moja ya hatua kubwa niliyofikia, namshukuru Mungu maisha yanazidi kusogea,” alisema Ommy.