Waziri wa habari nchini Ethiopia ameilaumu Eritrea kwa kuanzisha mapigano kati ya nchi hizo mbili ambayo yalianza siku ya Jumapili.
Ameiambia BBC kuwa wanajehsi wa Ethiopa wamefanikiwa kukabiliana na tisho hilo na kuongeza kuwa wamesababisha uharibifu mkubwa kwa wanajeshi wa Eritrea.

Image captionJeshi la Ethiopia

Awali Eritrea iliilaumu Ethiopia kwa kuanzisha mapigano hayo ambayo yalitokea katika eneo la mpaka linalotumiwa na nchi hizo zote karibu na mji wa Tsorona.
Uhusiano kati ya Eritrea na Ethiopia ni mbaya zaidi na mnamo miaka ya tisini, uhasama mpakani ulisababisha vita vya miaka miwili.