Rais wa Marekani, Barack Obama amesema hakuna ushahidi kuwa aliyetekeleza mashambulizi kwenye klabu ya usiku mjini Orlando alikuwa sehemu ya mpango mkubwa wa mashambulizi.

Obama ameeleza shambulio hilo lilisukumwa na msimamo binafsi wa mshambuliaji huyo na hakuna ushahidi kuwa Omar Mateen alipata maelekezo kutoka nje kutekeleza mauaji.
Mkurugenzi wa shirika la kijasusi FBI,James Comey amesema kuna ishara kuwa Mateen alishawishika kupitia mitandao ya intaneti.Lakini amesema haijulikani Mateen alikuwa akiunga mkono kundi gani la kigaidi.
Comey amesema muuaji huyo alieleza kuunga mkono kundi la wanamgambo wa IS na hasimu wa kundi hilo, Al Nusra la nchini Syria.