Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kitengo kinachoshughulikia Tsunami, Ardito Kodijat akifungua mafunzo hayo kwa kuwaeleza washiriki aina ya mafunzo ambayo watapatiwa. (Picha na Rabi Hume, MO Blog)

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues akitoa neno la ufunguzi kwa niaba ya UNESCO Tanzania na kueleza sababu ya kufanyika mafunzo hayo.

Mkuu wa Utafiti na Matumizi ya Hali ya Hewa kutoka Mamlaka ya Hewa nchini (TMA, Dk. Ladislauds Chang`a akizungumza jinsi TMA imejipanga kuendeleza kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Tsunami na kuwataka Watanzania kuwa na utaratibu wa kufatilia hali ya hewa nchini hasa katika kipindi hiki ambacho ni kuna mabadiliko ya tabia ya nchi.

Baadhi ya washiriki ambao wameshiriki katika mafunzo hayo ambayo yanataraji kufanyika kwa siku tano.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leonard Chamuriho akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo yanayohusu kuwapa elimu washiriki ya kuhusu Tsunami. (Picha na Rabi Hume, MO Blog)

 Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja. (Picha na Rabi Hume, MO Blog)
Watanzania wapata fursa ya kushiriki mafunzo kuhusu Tsunami
Kutokana na kuwa na athari kubwa ambazo zimekuwa zikisababisha majanga makubwa, Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limeandaa mafunzo ya siku tano ambayo yatashirikisha watu mbalimbali nchini ili kuwapa elimu kuhusiana na majanga.
Akizungumzia Mafunzo hayo, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues alisema kupitia mafunzo hayo yatawasaidia washiriki kupata elimu kuhusiana na Tsunami ikiwa ni pamoja na madhara ambayo yanasababishwa na hivyo ni matarajio yao watakuwa mawakala wazuri kwa kusambaza elimu hiyo kwa Watanzania wengine.
"Watu wengi wamepoteza maisha tukumbuke Tsunami la Japan zaidi ya watu 20,000 walipoteza maisha kwahiyo tunataka mafunzo haya yasaidie kufahamu ni kwa kiasi gani Tsunami linakuwa na madhara hata kama limetokea mbali na hapa," alisema Bi. Rodrigues.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dk. Leonard Chamuriho alisema ni vyema kwa watanzania kupata elimu hiyo kutokana na madhara ambayo yamekuwa yakitokea ikiwemo Tsunami la mwaka 2004 ambalo lilitokea eneo lililombali na bahari ya Hindi lakini lilisababisha athari nchini na kusababisha vifo vya waogeleaji watano.
"Mafunzo haya yanatakiwa kufanyika kwa wananchi wote na mwezi Septemba yatafanyika mengine na yatahusisha watu wengi lengo kila Mtanzania ajue nini cha kufanya siku athari zikitokea wajue nini wanafanya ni muhimu kwa kila mtu kujua athari za Tsunami hata likitokea mbali," alisema Dk. Chamuriho.
Na Rabi Hume, MO Blog