Hillary Clinton anawania urais akiungwa mkono na Barrack Obama.
Obama alimuidhinisha rasmi katika kongamano la chama cha Democrat.

Image copyrightREUTERS
Image captionObama na Clinton

''Hakujakuwa na mwanamume au mwanamke ,sio mimi wala Bill Clinton hakuna aliyefuzu zaidi ya Hillary Clinton'', aliuambia umati wa watu.
Walikumbatiana na kuonekana kwamba walikuwa marifiki wa jadi .Lakini haijakuwa hivyo .

Image copyrightGETTYIMAGES
Image captionClinton

Alipogundua kwamba huenda asishinde dhidi ya Obama miaka iliopita bi Clinton alimfanyia kampeni bwana Obama.
Aliposhinda urais Obama alimteua bi Clinton kama waziri wa maswala ya kigeni.

Image copyrightGETTY
Image captionObama na Clinton

Haikuwa rahisi kwani baadhi ya wasaidizi wake walishindwa kujirekebisha ili kuingiliana na uongozi wa Obama.