Rais wa China Xi Jinping anataka kuimarisha majeshi ya nchi yake huku taifa hilo likiendelea kudhihirisha ubabe sana kuhusu umiliki wa maeneo ya bahari Kusini na Mashariki mwa China.
Ndege hizo za J-20 zimeundwa na kampuni ya Chengdu Aircraft Industries Group, ambayo ni kampuni tanzu ya shirika la ndege la China ambalo kwa Kiingereza hufahamika kama Aviation Industry Corporation of China.
Baadhi wamelinganisha ndege hizo na ndege aina ya F-22 Raptor za Lockheed Martin.
Mchanganuzi wa masuala ya ndege Bradley Perret amesema ndege hiyo "bila shaka ni hatua kubwa katika uwezo wa kivita wa China".
Ndege ya kwanza kabisa ya kubeba mizigo mizito ambayo imetengenezewa nchini China, ndege ya Y-20, pia imezinduliwa katika maonesho hayo.
Ndyingine zinazotarajiwa ni ndege kubwa ya AG-600 ya kusaidia katika uokoaji na kushika doria baharini.
Aidha, ndege ya kivita ya kuangusha mabomu kwa jina Xian H-6K na helikopta ya kutekeleza mashambulizi ya Changhe Z-10K zitazinduliwa.
0 Comments