Waziri mkuu wa India Narendra Modi ametangaza kuwa noti ya Rupee 500 na ile ya 1000 zitaondelewa katika mfumo wa fedha kwa siku moja.
Hatua hiyo ya kushangaza ni mijawapo ya harakati za kukabiliana na Ufisadi pamoja na ukopeshaji wa fedha wa haramu alisema katika runinga.

Benki zitafungwa siku ya jumatano huku huduma za mashine za kutoa pesa za ATM zkisitishwa.
Noti mpya za rupee 500 na 2000 zitawekwa katika mfumo wa fedha ili kuchukua mahala pake noti hizo zilizoondolewa.
Ulanguzi wa fedha na ufisadi ndio vikwazo vikuu katika kukabiliana na umasikini ,alisema Modi.watu wataweza kubadilisha fedha noti zao za zamani na mpya katika benki katika kipindi cha siku 50 na kwamba fedha hizo hazitatumika tena.
Tangazo hilo liliwashinikiza raia kote nchini kuelekea katika mashine za ATM zinazotoa noti za rupee 100 katika hatua ya kutokosa fedha katika kipindi cha siku kadhaa zijazo.