MTENDENI, ZANZIBAR: Wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar leo wamevamia Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho yaliyopo eneo la Mtendeni visiwani humo wakitaka kufahamu hatma ya maamuzi yao ya Okt 25, 2015, ambapo chama hicho kinadai kilishinda uchaguzi kabla ya kufutwa.

Wafuasi wa CUF wakiwa wamekusanyika kwenye ofisi za chama hicho.