Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka  Gambo pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro wakisiliza mafunzo elekezi ya viongozi wa mkoa wa Arusha.








Na Imma Msumba, Arusha


Viongozi wa Mkoa wa Arusha wameshauriwa kuwajibika katika majukumu yao huku wakifuata kanuni na sheria mbalimbali za utumishi wa umma ili kuongeza ufanisi katika maeneo yao ya kazi huku wakileta maendeleo kwa mkoa.
Akifungua mafunzo elekezi kwa viongozi hao  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema viongozi wa mkoa wa Arusha wanatakiwa kuongeze mahusiano katika maeneo yao ya kazi baina yao na watumishi wachini yao.


Amesema lengo kubwa nikuondoa migongano inayojitokeza baina ya viongozi na watumishi hao ambayo inapelekea kudhorotesha utendaji  wa kazi katika maeneo yao na kuongezeka wimbi la uwonevu kwa watumishi wao.


Aidha amewataka viongozi hao wasimamie uwajibikaji wa watumishi katika maeneo ya kazi kwa kufuata taratibu za majukumu yao.
Akisisitiza zaidi kwa kuwataka viongozi kutekeleza maelekezo yanayotolewa na ngazi za juu serikalini kwani mengi yanakuwa ni miongoni mwa shughuli zao za kila siku na hii itaongeza utii kwa viongozi serikalini.
Nae katibu tawala wa mkoa  Richard  Kwitega amesema mafunzo hayo niyakukumbushana majukumu kwa viongozi hao huku wakipitia maeneo mbalimbali ikiwemo wajibu na majukumu ya viongozi,usimamizi wa Rasilimali watu sehemu za kazi napia kupitia kanuni na maadili ya viongozi na utumishi wa umma.
Amesema mafunzo hayo yatakuwa ya siku 2 huku yakishirikisha baadhi ya viongozi kutoka TAMISEMI.




Mkuu  wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro na Mkuu wa Wilaya ya Monduli Idd Kimanta wakisikiliza mafunzo ya viongozi wa Mkoa wa Arusha yaliyotolewa kwa lengo lakukuza uwelewa.



Kutoka kushoto ni Meya wa Jiji la Arusha Mh: Calist Lazaro pamoja na viongozi wa Mkoa wa Arusha waliohudhuria mafunzo elekezi kwa viongozi wa mkoa wa Arusha.


Imma Msumba
Director
Phone.0762 561399 / 0782 515566 / 0712 073737
P.o.box 12447
Arusha,Tanzania
www.msumbanews.com

2017-05-04 8:58 GMT+03:00 Dixon Busagaga :

Wageni wa meza kuu wakifurahia jambo wakati wa kuanza kwa fainali ya mashindano ya Habibu cup katika uwanja wa Cleopa Msuya wilayani Mwanga.
Kikosi cha timu ya Kifaru kikipasha misuli joto.
Kikosi cha timu ya Nyerere kikipasha misuli joto.
Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali za Mashindano ya Habibu Cup ,Thabit Mndeme akisalimiana na wachezaji wa timu ya Nyerere.
Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali za Mashindano ya Habibu Cup ,Thabit Mndeme akisalimiana na wachezaji wa timu ya Kifaru.
Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali kati ya timu za sekondari za Nyerere na sekondari ya Kifaru,Thabit Mndeme akizungumza kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali baina ya timu hizo mbili.
Kikundi cha ushangiliaji cha timu ya Nyerere .
Kikundi cha ushangiliaji cha timu ya Kifaru.
Sehemu ya hekaheka katika mchezo huo wa fainali.
Mchezaji wa timu ya Sekondari ya Kifaru akipiga penati iliyopelekea ushindi wa jumla ya bao 5 kwa 3 kwa timu ya Kifaru katika mchezoo wa fainali dhidi ya timu ya sekondari ya Nyerere .
Baadhi ya mashabiki walijitokeza kushuhudia michezo ya fainali katika mashindano hayo.
Mgeni rasmi Zuhura Mndeme akielekea katika uwanja wa mchezo wa Netiboli kwa ajili ya ufunguzi ya kuanzisha fainali ya mchezo huo kati ya timu ya Green Bird Collage na Sekondari ya Usangi Girls Day.
Timu ya Netiboli ya Shule ya sekondari ya Usangi Girls Day
Timu ya Green Bird Collage.
Mgeni rasmi kwa upande wa mchezo wa Netiboli ,Zuhura Mndeme akisalimiana na wachezaji wa timu ya Green Bird Collage.
Mgeni rasmi kwa upande wa Netiboli,Zuhura Mndeme akisalimiana na wachezaji wa timu ya Sekondari ya Usangi Girls Day.
Mwamuzi wa mchezo huo wa fainali akimkaribisha mgeni rasmi Zuhura Mndeme kufungua rasmi mchezo huo wa fainali.
Mgeni Rasmi Zuhura Mndeme akirusha mpira kwenye mlingoti wa goli wakati wa ufunguzi rasmi wa mchezo wa faiali ya Netiboli.
Mchezo wa fainali ukiendelea baina ya timu ya Green Bird Collage na Sekondari ya Usangi Girls Day mchezo uliomalizika kwa timu ya Green Bird kutangazwa malkia mpya wa mchezo huo baada ya kushinda kwa point 17 kwa 15 za Usangi Girls.
Mshindi wa kwanza katika mbio za Habibu Marathon Km 21 Musa Hassan akipokelewa baada ya kuhitimisha mbio katika uwanja wa Cleopa Msuya wilayani Mwanga.
Mshindi wa Pili katika Mbio za Habibu Marathon Peter Michael akihitimisha mbio hizo katika uwanja wa Cleopa Msuya.
Washindi Sita bora katika mbio za Habibu Marathon 2017 wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa mbio hizo.
Mgeni rasmi katika mashindano ya Habibu Cup ,Thabit Mndeme akikabidhi kombe la ubingwa wa mashindano hayo kwa Nahodha wa timu ya soka ya Kifaru ,Zuber Zuber mara bada ya timu hiyo kujinyakulia ubingwa wa mashidano hayo kwa mara ya pili mfululizo.
Wachezaji wa timu ya soka ya Kifaru wakishangilia mara baada ya kukabidhiwa Kombe la ubingwa.
Mgeni rasmi katika mashindano ya kumbukumbu ya Habibu Mndeme ,Thabiti Mndeme akimkabidhi kikombe cha umalkia wa mchezo wa netiboli wa timu ya Green Bird Collage .
Mgeni rasmi katika mashindano ya kumbukumbu ya Habibu Mndeme ,Thabiti Mndeme akimvisha medali mshindi wa kwanza wa mbio za Habibu Marathon Km 21 ,Musa Hassan.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.