Nini hufanyika kukikosekana mshindi wa moja kwa moja katika uchaguzi mkuu?
Chama chenye wabunge wengi ndicho pekee huunda serikali?

Si lazima. Chama chenye wabunge wengi baada ya kura zote kuhesabiwa maeneo yote 650, huwa kinatangazwa mshindi na kiongozi wake huwa waziri mkuu. Lakini hili huenda lisifanyike wakati huu kwa kuwa chama kilichoshinda hakina wingi wa wabunge. Inawezekana kwa chama kilichomaliza cha pili kuunda serikali.
Mtu hushinda vipi uchaguzi?
Njia rahisi zaidi kwa mtu kuwa waziri mkuu ni chama chake kupata wingi wa wabunge katika Bunge la Commons - kuwa na wabunge wengi kuliko wabunge wote wa vyama hivyo vingine wakijumlishwa.
Unahitaji wabunge wangapi kuwa na wingi?