Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani anawaalika wananchi katika halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga, Tanzania.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika Agosti 5, 2017 eneo la Chongoleani jijini Tanga ambapo utahudhuriwa na waasisi wa mradi huo mkubwa - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni.