RAIS Samia Suluhu Hassan amesema serikali imetia saini mkataba wa makubaliano ya ukarabati na maboresho ya uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal II uliojengwa na Wafarasa ili kuwa na muonekano zaidi ya ule wa Terminal III.

 

Rais Samia amesema hayo  leo Februari. 20 muda mchache baada ya kuwasili akitokea Ubelgiji baada ya ziara yake katika nchi hiyo na Ufaransa.