Ofisi ya waziri mkuu wa nchini Uingereza, Downing Street imethibitisha kuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo Boris Johnson anakutana na rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky katika mji mkuu Kyiv.

Msemaji wa ofisi ya Waziri mkuu amesema : “Waziri mkuu amesafiri kwenda Ukraine kukutana na Rais Zelensky binafsi ili kuonyesha ushirikiano na watu watu wa Ukraine.

"Watajadili uungaji mkono wa Uingereza wa muda mrefu kuisaidia Ukraine na waziri mkuu atatenga fedha usaidizi mpya wa kifedha na kijeshi.