Rihanna ameiambia BBC kuwa amefurahia kuandika upya sheria za mitindo kama mama, akisema "alikataa kununua nguo za ujauzito".

"Nilijiambia ninataka kufanya kila kitu ninachofanya katika mitindo wangu ," alisema. "Nataka tu kufanya mambo kwa njia yangu na kila wakati nibadilishe na kuweka mtazamo wangu juu yake.

"Nilifikiria nikasema nataka kuona kama chochote kinachofaa kitafanikiwa nitakifanya, na hiyo ilinifanya nijipe changamoto ya kuwa mjanga kwa mtindo," aliongeza.

j
Image caption: Rihanna, pichani akiwa na ujauzito wa mtoto wake wa kwanza mnamo 2022

Alikuwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa ushirikiano wake hivu karibuni na kampuni ya mavazi ya Puma.

Mshindi huyo wa tuzo nyingi za Grammy ana watoto wawili wa kiume na rapper A$AP Rocky - RZA Athelaston Mayers, aliyezaliwa mwaka wa 2022, na Riot Rose Mayers, aliyezaliwa mwaka wa 2023.