Jeshi la Thailand lilaulaumua Cambodia kwa kuvunja makubaliano mapya ya kusitisha mapigano, yaliyotiwa saini baada ya wiki kadhaa za mabishano yaliyopelekea karibu watu milioni moja ykukimbia makazi yao.

Jeshi la Thailand limesema kuwa zaidi ya ndege zisizo na rubani (UAV) 250 zilionekana zikiruka kutoka upande wa Cambodia Jumapili usiku.

Katika taarifa, jeshi la Thailand limesema kwamba hatua ya Cambodia “ni ukiukaji wa hatua zilizokusudiwa kupunguza mvutano”, huku ikionekana kutokubaliana na masharti ya kusitisha mapigano.

Jeshi hilo pia limesema linaweza kufikiria upya kuhusu kuachiliwa kwa wanajeshi 18 wa Cambodia waliokuwa wameshikiliwa Thailand tangu Julai.

Cambodia bado haijatoa kauli yoyote kuhusu madai haya.

Hii inatokea masaa machache tu baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi, kusifu hatua ya kusitishwa kwa mapigano iliyofikiwa kwa juhudi kubwa, na Rais wa Marekani, Donald Trump

China imesifu pia kumalizika haraka kwa mzozo na kwa haki kwa makubaliano muhimu.