Rais aliyeondolewa madarakani wa Korea Kusini Yoon Suk Yeol amepatikana na hatia ya kutumia vibaya madaraka na kughushi nyaraka kuhusu jaribio lake la sheria ya kijeshi lililoshindwa mwaka 2024.
Mahakama ya Seoul sasa inajadili kama pia alizuia utekelezaji wa haki kwa kukwepa kukamatwa. Waendesha mashtaka wameomba ahukumiwe kifungo cha miaka 10 jela kwa mashtaka haya.
Hii ni hukumu ya kwanza kati ya hukumu nne zilizotolewa katika kesi zilizohusishwa na amri yake ya kushangaza ya sheria ya kijeshi.
Ingawa ilikuwa ya muda mfupi, hatua hiyo iliiingiza nchi katika msukosuko, na kusababisha maandamano huku wabunge wakikimbilia bungeni ili kubatilisha uamuzi wa Yoon.
Uamuzi wa Ijumaa unatoa vidokezo kuhusu jinsi kesi zingine za Yoon zinavyoweza kwenda.
Mashtaka yanaanzia matumizi mabaya ya madaraka hadi ukiukaji wa sheria za kampeni.

0 Comments