Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa Iran “haijawahi kuomba kusitishwa kwa vita, wala hata kuomba mazungumzo na Marekani.”

Kauli hiyo inafuatia kauli ya awali ya Donald Trump aliyedai kuwa Iran ilitaka kufanya mazungumzo, lakini yeye hakuwa tayari kuyakubali kwa sababu masharti yake hayatekelezeki.

“Hatuoni sababu yoyote ya kuzungumza na Wamarekani, kwa sababu tulikuwa tayari tunazungumza nao wakati wao waliamua kutushambulia,” ameiambia CBS News.

Ameongeza kusema: “Hii ni vita vilivyochaguliwa na Rais Trump pamoja na Marekani, na sisi tutaendelea kujilinda.”